Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Sunday, June 23, 2013

BALOZI WILFRED JOSEPH NGIRWA ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI WA BARAZA LA SHIRIKA LA CHAKULA NA KILIMO

Shirika la Chakula na Kilimo FAO, Ijumaa katika Kikao chake cha 38, lilimchangua Balozi Wilfred Joseph Ngirwa, kuwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la FAO, kwa kipindi cha miaka miwili ijayo June 2013 hadi June 2015.
Balozi Wilfred Ngirwa, amechaguliwa kushika  nafasi hii ya Mwenyekiti wa kujitegemea  wa Baraza katika maana ya Mwenyekiti aliye huru asiyegemea upande wowote, kwa shindi wa asilimia 96 kati ya kura zote zilizopigwa na wajumbe wa Baraza 154, kura za ndio zikiwa 146, kura turufu  7 na kura za hapana 1( moja) .
Balozi Wilfred Ngirwa alizaliwa Tanzania mwaka 1948 katika familia ya kawaida ya Watanzania,Bukoba Mkoani Kagera.  Ni mtalaam katika uwanja wa Kilimo na uchumi, kazi aliyoifanya wa muda wa miaka 38 , ambamo huduma yake ilitambulwia vyema hasa kwa mchango wake kama Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Tanzania na katika  Mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa yanayohusika na huduma kwa Mkulima, ambayo ni Shirika la Chakula na Kilimo(FAO) Shirika la Mfuko wa Maendeleo katika Kilimo(  IFAD), na Shirika la Mpango wa Chakula  (WFP).  Na pia kama Mwakilishi wa Tanzania katika mashirika hayo,uwakilishi uliompa heshima ya kuwa  Balozi.
Katika Khafla ya kumpongeza  Balozi Ngirwa, iliyoandaliwa na Ofisi ya Ubalozi wa  Tanzania nchini Italy, Waziri wa Kilimo Tanzania,  Mheshimiwa Waziri Christopher Kizza , alisema, ushindi wa Balozi Ngirwa katika kinyanyang’iro cha cheo hicho, umekuwa ni ushindi na heshima kubwa kwa  Afrika,  na hususani kwa Watanzania wote.  Na hivyo ushindi huu ni changamoto inayodai hasa tanzania kwa ujumla kuendelea kuishi kwa  amani na utulivu, katika kudumisha heshima ya Tanzania kwenye  ngazi za Kimataifa, na kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania, na hasa Wakulima na wafugaji vijijini.
Waziri aliomba ushirikiano wa karibu na Mwenyekiti Mpya wa Baraza la FAO,akisema, ingawa kwa cheo chake hakifungamani na upande  wowote, bado Afrika  inatazamia kunufaika zaidi na mchango wake, katika kubadili maisha ya mkulima wa Afrika hasa kwa kutokana na uzoefu wake katika maisha yake ya kawaida ya mkulima  wa Afrika Vijijini.  
Na Balozi James  Nsekela , katika hotuba yake fupi kwa Khafla hiii, alionyesha furaha yake kwamba Kupitia Balozi Ngirwa , Tanzania imeaminiwa kuliongoza Shirika la FAO.  Aliiaja kazi hii kuwa ni nzito na nyeti yenye kuhitaji weledi na ushirikiano wa karibu na watendaji wengine. Vivyo katika Khafla hii alikuwepo Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Zanzibar, Dr. gharib .
Na Balozi Ngirwa, alitoa shukurani zake za dhati kwa  Rais wa Jamhuri ya Tanzania, Rais Jakaya Kikwete,  kwa kuidhinisha jina lake liwakilishwe FAO, kama mgombea wa cheo  cha Mwenyekiti wa kujitegemea katika Baraza la FAO. Na pia aliwashukuru wote, waliomtia moyo wa kugombea kiti hicho.  Na kwamba akiwa katika cheo hiki kipya atafanya kazi zake katika misingi ya imani yake kwamba , FAO ni shirika ambamo misingi ya maamuzi yake imesimikwa katika misingi ya makubaliano ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa. Na hivyo, mamlaka yake yatazingatia rejea msingi zilizotajwa katika nyaraka za FAO, na Mpango wa Kidharura wa Utendaji  kama ilivyo ainishwa katika hati za makubaliano za Fao.
Balozi Ngirwa anaanza Kazi yake Mpya Jumatatu 24 June 2013, katika makao makuu ya FAO , Mjini  Roma. 

Na Mrs. Tabitha Janeth Mhella
 BALOZI NGIRWA AKIPONGEZWA NA WAZIRI WA WIZARA YA KILIMO WA TANZANIA MHESHIMIWA CHISTOPHER KIZZA.



 WAZIRI WA KILIMO TANZANIA
.
  WAKATI UCHAGUZI UKIENDELEA. TOKA KUSHOTO NI MH. BALOZI NGIRWA KATIKATI NI BALOZI WA TANZANIA ITALY MH. JAMES MSEKELA NA KULIA NI WAZIRI WA KILIMO TANZANIA MH. CHRISTOPHER KIZZA.
 BALOZI NGIRWA AKIPONGEZWA.
 TIMU YA TANZANIA ILIYMSINDIKIZA BALOZI NGIRWA SIKU YA UCHAGUZI.

                                     
 WAKATI WA CHAKULA CHA USIKU PAMOJA NA MH. BALOZI NGIRWA.
 BALOZI NGIRWA AKIPATA PICHA YA PAMOJA WAKATI WA CHAKULA CHA USIKU CHA KUMPONGEZA KILICHOANDALIWA NA MH. BALOZI JAMES MSEKELA.


 WAHESHIMIWA WAKIGONGESHA GLASI KUMPONGEZA BALOZI NGIRWA.




 KUTOKA KUSHOTO NI KATIBU WA JUMUIYA YA WATANZANIA ITALY NDG. ANDREW CHOLE MHELLA NA KATIBU MSAIDIZI WA JUMUIYA HIYO BI. DIANA PAUL OLOTU.

Picha Zote zimepigwa na Mr. Msemo toka ubalozi wa Tanzania Italy.

No comments:

Post a Comment