Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Saturday, October 5, 2019

MKUTANO WA UCHAGUZI WA VIONGOZI WAPYA WA JUMUIYA YA WATANZANIA ROMA WAFANA

Mkutano wa Watanzania waishio Roma uliofanyika tarehe 29 September 2019 kwenye ukumbi wa ubalozi wa Tanzania nchini Italy ulikuwa na mafanikio sana. Mkutano huu ambao uliandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Italy, chini ya balozi Watanzania nchin Italia, Mh. George Kahema Madafa pamoja na Jumuiya ya Watanzania Roma, ulikuwa na agenda kuu mbili; ya kwanza, ni kuchagua viongozi wapya, baada ya muda wao kuisha; pili kusikiliza ujumbe wa serikali kutoka kwa Mh. Balozi juu ya maswala mbalimbali ambayo yanatugusa sisi Watanzania tuishio ughaubuni.

Kwenye Mkutano huu, viongozi waliochaguliwa ni hawa wafuatao;
1. Leonce Uwandameno (Mwenyekiti)
2. Anastasia Lubangula (Katibu)
3. Irene Mutungi Kaigarula (Mweka Hazina)

Wajumbe wa Kamati kuu waliochaguliwa ni:
1. Andrew Chole Mhella
2. Mwishehe Abeid
3. Pendo

Picha zote zimeletwa kwa isani ya Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti Mstaaafu, 
Ndugu Andrew Chole Mhella.












Sunday, September 15, 2019

Sunday, September 30, 2018

Thursday, November 16, 2017

TANGAZO LA MSIBA MJINI NAPOLI - ITALY.


Jumuiya ya Watanzania Roma imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba kutoka Napoli za ndugu JUMANNE MOHAMED MKASI ajulikanaye na wengi kama "TUESDAY". Marehemu Tuesday, ambaye alikuwa mgonjwa kwa muda mrefu alifariki jana asubuhi tarehe 15/11/2017 hospitalini mjini Napoli alipokuwa amelazwa kwaajiri ya matibabu. Marehemu kwa Tanzania ni mkazi wa kata ya Manzese, Mtaa wa Mnazi Moja mjini Dar -es -Salaam.

Uongozi wa Jumuiya unapenda kuwafahamisha watanzania mjiini Roma kuwa jumamosi ya tarehe 18 November 2017, kuanzia saa kumi jioni, kutakuwa na mkutano wa kuchangisha fedha kwaajiri ya kuhusafirisha mwili wa marehemu kwaajiri ya mazishi nchini Tanzania. Mkutano utafanyika kwenye mtaa wa Via Principe Amedeo 70 (Indian Restaurant) maeneo ya Termini Station.

Kwa wale mtakaoshindwa kufika siku ya Jumamosi kwa sababu zilizo nje ya uwezo wenu, mnaombwa muwasiliane na Mwenyekiti, Andrew Chole Mhella, Ndugu Kondela Buhire au ndugu Mwishehe kwaajiri ya michango yenu.

Upatapo ujumbe huu tafadhali unaombwa umfahamishe na mwenzako.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu "Tuesday" mahali pepa peponi. Amen.
Mwenyekiti,
Andrew Chole Mhella

Tuesday, May 2, 2017

AMBASSADOR WILFRED JOSEPH NGIRWA HONOURED BY UN FOOD AND AGRICULTURE ORGANIZATION

Ambassador Wilfred Joseph Ngirwa was honoured by unvailing hi portrait in the UN Food and Agriculture Organization in Rome, during the Session of the FAO Council which was held from 24-28 April 2017.

Ambassador Ngirwa who is the current Independent Chairperson of the UN FAO Council, was unanimously elected unopposed by Member Nations of FAO to serve in his capacity in 2013. Previously, he was the Ambassador of Tanzania as Permanent Representative to the UN Food Agencies in Rome, Italy.

The Ambassador of Tanzania H.E. George Kahema Madafa represented Tanzania in the FAO Council Session and witnessed the unvailing of portrait ceremony of Ambassador Ngirwa.

                                                               THE PORTAIT



HON. AMBASSADOR NGIRWA AND H.E. AMBASSADOR GEORGE KAHEMA MADAFA
                                                   

HON. NGIRWA TOGETHER WITH HIS WIFE


HON. NGIRWA TOGETHER WITH


 

Sunday, November 6, 2016

WATANZANIA MJINI ROMA WAMPONGEZA NA KUMUAGA MAMA TABITHA JANETH MHELLA

 
Watanzania mjini Roma, jana jumamosi tarehe 05 Novemba 2016, walikusanyika kwenye sherehe ya kumpongeza na kumuaga Mama Tabitha Janeth Mhella (Mama Mhella)  ambaye tarehe 31 Oktoba 2016.

Mama Mhella ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican amekuwa mwafrika  wa kwanza kutunukiwa zawadi ya heshima  na Papa Francis , kwaajili ya utendaji mzuri wa kazi na huduma ya Kanisa.

Sherehe hii ambayo ilifana sana, iliudhuliwa na Watanzania kutoka kila kona ya Roma.
Kwenye hafla hiyo, Mama Mhella, alipata fursa ya kuwashukuru Watanzania wote kwa upendo waliomuonyesha tokea alipowasili mjini Roma mwaka 1992 na pia kuwashukuru kwa ushirikiano na upendo  waliompa kwenye kipindi cha miaka 24 cha uwepo wake mjini Roma.

Vile vile, kwa niaba ya Watanzania mjini Roma, Mheshimiwa kaimu Balozi, Mr. Salvatori Mbilinyi ambaye alikuwa mmoja ya washiriki wa sherehe hiyo, alimpongeza mama Mhella kwa kustahafu kazi na zaidi kumshukuru kwa upendo wake, busara zake na ukaribu aliokuwa nao na Watanzania wote.  Mh. Kaimu balozi alimalizia kwa  kumtakia Mama Mhella safari njema ya kurudi nchini Tanzania.





















Sunday, September 18, 2016


MICHANGO YA HIARI KWA AJILI YA WAHANGA WA TETEMEKO LA ARDHI - KAGERA


UONGOZI WA JUMUIYA YA WATANZANIA ROMA UNAPENDA KUWAFAHAMISHA WATANZANIA WOTE MUISHIO ROMA KUWA JUMAMOSI YA TAREHE 24/09/2016 KUTAKUWA NA MKUTANO WA KUCHANGIA WAHANGA WA TETEMEKO LA ARDHI MJINI MKOANI KAGERA NCHINI TANZANIA. TUNAOMBA MFIKE KWA WINGI ILI TUWEZE KUFANIKISHA ZOEZI ILI. MKUTANO UTAFANYIKA KWENYE INDIAN RESTAURANT ILIYOPO VIA PRINCIPE AMEDEO, MAENEO YA TERMINI STATION.
UPATAPO UJUMBE HUU TAFADHALI MJULISHE NA MWENZIO.

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE.


ANDREW CHOLE MHELLA

MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WATANZANIA ROMA

Thursday, June 16, 2016