Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Sunday, April 13, 2014

MKUTANO WA WATANZANIA ROMA WAFANA

 
Watanzania waishio Mjini Roma, Jana jioni tarehe 12 aprili 2014 walikutana kwenye ukumbi wa Wahindi uliopo Via Principe Amedeo mjini Roma, kujadili maswala mbalimbali yanayowagusa Watanzania kwa ujumla. Uongozi wa Jumuiya ya Watanzania Roma, ambao ndio ulichukua jukumu la kuongoza mkutano huu, ulikuwa  na lengo kuu la kuwakumbusha Watanzania waishio mjini Roma umuhimu wa Kujiunga na Jumuiya. Mwenyekiti na Katibu walisisitiza sana kwenye kuwaelimisha wale ambao hawajafunguka, juu ya umuhimu wa kujiunga na Jumuiya. Katika kutoa motisha, Katibu, ndugu Andrew Chole Mhella alieleza kuwa, Jumuiya ni chombo muhimu sana kwa sisi Watanzania tuishio ughaibuni, aliendelea kusema kuwa ni chombo cha kuwakutanisha Watanzania ili waweze kufahamiana, kusaidiana, na kutatua matatizo mbalimbali ya yanayowapata. Kwa hiyo basi kwa kujiunga na jumuiya aliendelea Katibu, utatambulika rasmi kuwa ni mmoja wa wanajumuiya na utakuwa na haki ya kusaidiwa kama mwanajumuiya. Haki ambayo watanzania wengi mjini Roma wanaikosa. Katibu alendelea kusema kuwa hapa mjini Roma, Watanzania wengi wamekuwa wakiutafuta na wamekuwa wakiona umuhimu  wa Jumuiya pale tu wanapokuwa na matatizo, kama vile ugonjwa , kifo, shida ya passport na na matatizo mbalimbali ya kisheria.
Kabla ya kufunga kikao, Katibu aliwaomba wale wote wanataka kujiunga na jumuiya wamwandikie e-mail: watanzaniaroma@yahoo.it au kumpigia Katibu simu kwa namba hii 3391597134 ili aweze kuwapa copy ya Katiba pamoja na fomu la kujiunga! Kikao kijacho kitakuwepo mwanzoni mwa mwezi tano. tarehe kamili mtatangaziwa.
 








No comments:

Post a Comment