Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Tuesday, February 11, 2014

JUMUIYA ZA WATANZANIA ITALY ZAUNDA KAMATI YA DIASPORA


Jumuiya za Watanzania Italy, kwa pamoja walifanya mkutano mkuu wa kihistoria siku ya jumamosi tarehe 8/2/2014.

 Mkutano huo uliofanyika mjini Napoli,ulikuwa na madhumuni matatu makubwa. 
kwanza kuimarisha mshikamano baina ya Jumuiya za Watanzania nchini Italy, na pili kuzungumzia kero na matatizo ya Watanzania wanaoishi Italy.Wajumbe walichangia yote yaliyokusanywa katika mikutano na vikao vya awali.

Yote yaliyojadiliwa yatafanyiwa kazi na kufikishwa kunakostahili kwa ufumbuzi wa kudumu.

Jambo kubwa la tatu, Wajumbe waliunda kamati ya pamoja ya diaspora yenye wajumbe kutoka NAPOLI,ROMA,MODENA,GENOVA NA PADOVA. Na kuweka majukumu. Wajumbe pia walimchagua:
 Ndugu Kagutta N.Maulidi  (Mwenyekiti)
 Ndugu Ricky JG.Bondo ( kaimu m/kiti)
Ndugu Andrew Chole Mhela (katibu) 
 Ndugu Mwinyimwaka Sarai (kaimu/katibu),
Ndugu LIlian Luhende (hazina)
Ndugu Abdulrahaman A.Alli (mjumbe)
Ndugu Erasmus Luhoyo (Mjumbe)
Ndugu Livinus Mwereke (Mjumbe)
Ndugu Awadhi Sulaiman (Mjumbe)
Ndugu Judith Joseph  (Mjumbe)
Ndugu Zacharia Madjid Mhessa (Mjumbe)

Wajumbe wa mkutano wamependekeza kuwa baada ya kipindi cha miaka miwili  utafanyika mkutano wa kutathmini utendaji wa kamati kwa  ujumla.
Mwisho mwenyekiti wa jumuiya ya Watanzania Italy mh Abdulrahaman A.Alli aliwapongeza baadhi ya viongozi na wajumbe kwa kuwatunukia shahada za uongozi bora na uhadilifu.
Source: Jumuiya ya Watanzania Italy
(www.watanzaniaitalia.blogspot.it)
Pichani Mwenyekiti wa jumuiya ya Watanzania Italia Mh Abdulrahaman A.Alli(aliyeshika cheti)  akimtunukia cheti cha uadilifu na uongozi bora Katibu wa Jumuiya ya Watanzania Roma Mh. Andrew Chole Mhela. 

Mwenyekiti wa kamati ya Diaspora Mh. Kagutta N.Maulidi akionyesha cheti alichotunukiwa na mh Mwenyekiti kwa uadilifu na uongozi bora wa jumuiya ya Watanzania Italy .

Wajumbe wakifuatilia mkutano kwa makini


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Italia Mh Abdulrahaman A.Alli nae alikabidhiwa cheti cha uongozi bora, anaemkabidhi ni mwenyekiti wa jumuiya ya Watanzania Roma Mh.Erasmus Luhoyo. wengine ni Katibu Andrew Mhela(mwenye kitambaa shingoni) na wa pili ni Katibu mkuu mh Kagutta N.Maulidi na pembeni aliyevaa jacket ni katibu wa jumuiya ya watanzania wa Napoli Mjini Mh Livinus Mwereke.


viongozi katika picha ya pamoja


hii ndio kamati ya Diaspora



Mwenyekiti wa kamati ya Diaspora katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati.

Kaimu Mwenyekiti wa Diaspora Mh Ricky JG.Bondo akifafanua jambo kwa mjumbe ndugu Mohamed Mnondwa, baada ya kikao.

No comments:

Post a Comment