Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Sunday, December 15, 2013

MKUTANO WA MSIBA MJINI NAPOLI

 Watanzania leo walikutana chini ya uongozi wa Jumuiya ya Watanzania Italia, kupata taarifa rasmi ya kifo cha  marehemu ABDULLI ABUU ( HATIBU CLEAN HEART) na kupanga mikakati ya mazishi. Uongozi wa jumuiya ya Watanzania Italia uliongozwa na katibu mkuu wa Jumuiya  ndugu Kagutta N.Maulidi, akiwa pamoja na Katibu wa Napoli ndugu Livinus Mwereke na katibu mipango wa jumuiya ndugu Mohamed Abdulwahab, viongozi walito muhtasari wa kifo cha marehemu na wajihi wake,pamoja na hayo pia walitoa taarifa iliyotoka kwa wazazi wa marehemu kupitia kwa mwenyekiti wa jumuiya ambae kwa wakati huu yuko Tanzania kikazi. ilielezwa pia kuwa mwenyekiti wa jumuiya ya Watanzania Italia ndugu Abdulrahamani A.Alli atakuwa na kikao na wazazi wa marehemu  kesho  jumapili ili kuwapa taarifa na taratibu zinazofanywa na Watanzania chini ya Jumuiya  za Watanzania Italia.

Marehemu alifariki mjini Rome siku ya tarehe 8/12/2013. Tayari taarifa ya msiba imeshatolewa kwa Balozi wa Tanzania Italy uliopo Rome, Taarifa hizo zilifikishwa jana na Katibu wa jumuiya ya Watanzania Rome ndugu Endrew Mhela, baada ya kutambua mwili wa marehemu, hospitali na sehemu ulipo. Vilevile taarifa zilizoletwa na ndugu Mhela kuwa tayari amekwisha wasiliana na wakala wa usafiri kwa ajili ya kusafirisha mwili wa marehemu Hatibu cleanheart nyumbani Tanzania kwa mazishi.

Tayari michango imesha anza kukusanywa,ndugu Livinus Mwereke aliwahimiza Watanzania wote kujitolea zaidi ili kuharakisha taratibu za kusafirisha mwili ili kwenda na muda kabla haujapinduka mwaka. Taarifa zilisema pia kuwa Jumuiya ya Watanzania Rome watakuwa na mkutano na watanzania siku ya jumanne,vilevile Modena na Genova.  Kwa yeyote mwenye nia ya kuchangia kwa walioko mbali yaani nje ya Italy wanaweza kuwasiliana moja kwa moja na Katibu wa Jumuiya ya Watanzania Rome ndugu Mhella ambae ndie anaesimamia mpango mzima.

Mungu amlaze mahala pema peponi Ameen!!


mawasiliano: 0039 339 1597134

WATANZANIA WAKISIMAMA KIMYA KWA DAKIKA ISHARA YA HESHIMA NA KUMUOMBEA MAREHEMU KABLA YA KUANZA KWA MKUTANO.
Source:Jumuiya ya Watanzania Italy- www.watanzaniaitaly@blogspot.it

No comments:

Post a Comment