Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Sunday, January 29, 2012

HAPPY BIRTHDAY TANZANIAN COMMUNITY IN ROME

Timu ya Uongozi wa Jumuiya ya Watanzania Rome ambayo ilichaguliwa siku ya 30 Januari 2010. Kutoka kushoto ni Bw. Andrew Chole Mhella(Katibu) Bw.Erasmus Pindu Luhoyo (Mwenyekiti Msaidizi), Bw. Leonce Uwandameno (Mwenyekiti), Bw. Awadhi Suleiman ( Mweka Hazina) na Bi. Diana Paul Olotu(Katibu Msaidizi)

Hapa ni wakati kujadili katiba, kutoka kushoto ni ndugu Andrew Chole Mhella, katikati ni Mh. Andrew Kyabashasa ambaye alikuwa mwenyekiti wa mkutano wa uchaguzi na kulia ni Mgeni rasmi, Mh. Kaimu balozi Salvator Mbilinyi (Kutoka kwenye Kumbukumbu zetu)

Leo 30 Jan. 2012, Jumuiya ya Watanzania Roma imetimiza rasmi miaka miwili tangu kuanzishwa kwake mnamo 30 Januari 2010. Itakumbubwa na wengi kuwa siku kama leo kwenye ukumbi wa l'aggiustafesta, uliopo mtaa wa via cassalettico 6, eneo la cassia-Grottarossa, Watanzania kwa pamoja walikutana kujadili na kupitisha katiba. Siku hiyo hiyo watanzania hao walifanya uchaguzi wa viongozi ambao kwa kipindi cha miaka miwili wameongoza jumuiya. Kaimu Balozi Mheshimiwa Salvator Mbilinyi alikuwa mgeni rasmi siku hii ya kihistoria ya Watanzania Wahishio Rome. Kwenye mkutano huu Watanzania wafuatao walichaguliwa kuwa viongozi: Mwenyekiti( Leonce Uwandameno); Mwenyekiti Msaidizi(Erasmus Pindu Luhoyo); Katibu ( Andrew Chole Mhella); Katibu msaidizi ( Diana Paul Olotu); Mweka Hazina (Awadhi Suleiman) na Wajumbe (Bwana Boniface Mhella na Bi. Khadija Kirro).
Kulingana kifungu namba 5.2 cha katiba, kila baada ya miaka miwili, wanajumuiya wanapaswa kufanya uchaguzi wa viongozi wapya. Kutokana na viongozi wa sasa kumaliza kipindi chao cha uongozi, kutakuwa na uchaguzi wa viongozi wapya siku chache zijazo. Uongozi utawatambazia pale mipango yote itakapokuwa imekamilika.
Uongozi wa jumuiya unapenda kuwakumbusha watanzania wote kuwa uchaguzi utahusisha WANAJUMUIYA HAI TU. Wanajumuiya hai ni wale ambao wanashiriki kwenye vikao mbalimbali vya jumuiya na ambao wanashiriki kwenye kuchanga michango ya kila mwezi na michango mbalimbali ambayo inaidhinishwa na wanajumuiya wote na wale ambao hawajavunja kanuni za katiba.

Mungu Ibariki Jumuiya ya Watanzania Rome, Mungu ibariki Tanzania.

No comments:

Post a Comment