Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Friday, July 9, 2010

Zoezi la CCM kumpata mgombea urais Zanzibar lakamilika


Mh. Mohamed Shein


Mh. Balozi Ali Abeid Karume

Zoezi la Kumpata mgombea urais Zanzibar kupitia chama tawala cha CCM limekamilika leo ambapo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dr. Mohamed Shein ametoka kidedea kwa kupata ushindi mnono wa kura 117. Wagombea wengine wa CCM visiwani Zanzibar, Mh. Bilal alipata kura 54 na Mh.Nahodha kura 33. Washiriki wengine ambao walikuwepo kwenye kinyang'anyiro hicho ambapo mmoja wao alikuwa ni balozi wa Tanzania nchini Italy, Mh. Ali Abeid Karume,walishindwa kupata nasafi hiyo kwa kipindi hiki cha uchaguzi 2010. Uongozi wa Jumuiya ya Watanzania Rome kwa niaba ya wanajumuiya wake wote, unampongeza Mh. Dr. Mohamed Shein kwa kupata nafasi hii ya kugombea kupitia Chama cha Mapinduzi kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu utakao fanyika mwezi wa kumi na kuwapongeza pia wagombea wengine akiwemo balozi wetu hapa Italy Mh. Ali Abeid Karume kwa kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi hiyo. Itakumbukwa kuwa Jumuiya ya Watanzania Rome ni Jumuiya ambayo si ya Kisiasa lakini pia ni muhimu sana kuwapongeza viongozi wetu bila kujali vyama vyao vya siasa pale wanapopiga hatua ya kuleta maendeleo nchini Tanzania. Hii yote inaonyesha ukuaji wa demokrasia nchini Tanzania. Mungu Africa, Mungu Ibariki Tanzania.

No comments:

Post a Comment