Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Monday, April 28, 2014

SHEREHE YA KUADHIMISHA MIAKA 50 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR YAFANA MJINI ROMA

Watanzania nchini Italia, Jumamosi tarehe 26 Aprili 2014, walikutana mjini Roma kwenye ukumbi wa Ubalozi uliopo Viale Cortina d’Ampezzo 185, kusherehekea sikukuu ya kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Mgeni rasmi alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Dkt. James A. Msekela. Sherehe ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Jumuiya za Watanzania Italia, Maofisa wa Ubalozi na familia zao, Maofisa wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyoko Roma na familia zao pamoja na Watanzania waishio Italia.
                                            

Hii ndio ilikuwa keki ya Muungano
                   

Bi. Mary Mtemahanji, mwakilishi wa Jumuiya ya Watanzani Modena akiimba kwa furaha wakati wa kufungua champeign.


Bi. Zainab na Bw.Peter wakikata keki ya Muungano kwa pamoja.


.
Picha ya pamoja. Kushoto ni Katibu wa Jumuiya wa Watanzania Roma na pia Katibu wa Kamati ya Diaspora Italia Bw. Andrew Chole Mhella, katikati ni Bw. Peter na kulia ni Mjumbe wa Jumuiya ya Watanzania Roma Bw. Kondela Buhire.
Mheshimiwa Balozi Dkt. James Msekela akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Italia Bw. Abdulrahmani A.Ali.
Kutoka kushoto ni Bw. Karim Msemo, Ofisa wa Ubalozi Roma; Bw. Peter na Bw. Kondela Buhire, mjumbe wa Jumuiya ya Watanzania Roma.


Mh. Balozi akisalimiana na Katibu wa Jumuiya ya Watanzania Roma na Katibu wa Kamati ya Diaspora Italy ndugu Andrew Chole Mhella.
POZ KWA POZ



Wadada


Picha ya pamoja ya baadhi ya viongozi wa Jumuiya za Watanzania Italia na Ofisa wa Ubalozi.


PICHA ZINGINE ZITAFUATA BAADAE.
( Picha zote zimepigwa na Ndugu Karim Msemo)

No comments:

Post a Comment