Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Monday, May 14, 2012

Sherehe ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Roma yafana.



Kwa mbali Mama Tandika pamoja na Mama Mhella nao walikuwepo.



     Dj. Beka alizungukwa na mashine ya nguvu.

Ile sherehe ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyokuwa ikisubiriwa na wengi mjini Roma, ilifanyika jumamosi tarehe 12 Mei 2012.Sherehe ilifanyika kwenye ukumbi wa Karispera club 69, uliopo katikati ya mji mkuu Roma na kuudhuliwa na Watanzania wengi kutoka sehemu mbalimbali za Italia. Mgeni rasmi alikuwa balozi wa Tanzania nchini Italia, Mh. James Msekela, ambaye kwa mara ya kwanza alikutana na Watanzania kwa pamoja kutoka kila kona ya Italia. Kwenye sherehe hii, balozi Msekela aliishukuru Jumuiya ya Watanzania Roma kwa kuandaa sherehe hii muhimu kwa Taifa la Tanzania kutokana na dhumuni lake la kusherekea muungano ambao ni moja ya ngao ambazo tuliachiwa kama urithi na baba wataifa Mwalimu Julius kambarage Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume. Balozi Msekela pia aliwaelezea Watanzania kuwa amefurahishwa sana na umoja ambao ameuona kwenye siku chache toka kufika kwake nchini Italia na kuwaomba Watanzania waendelee na moyo huu wa ushirikiano maana ndio kitambulisho cha Tanzania nje ya nchi. Balozi alihaidi kushirikiana na hizi jumuiya za Kitanzania hapa Italy na kuwaomba wasisite kwenda kumuona pale watakapo kuwa wanaitaji ushauri na msaada wa aina yeyote toka ofisini kwake.

Mungu Ibariki Tanzania
( Picha na George Mayaka) zingine zitafuata muda si mrefu.


No comments:

Post a Comment