Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Sunday, November 20, 2011

MKUTANO MKUU WA JUMUIYA YA WATANZANIA ROME WAFANA




































































































































































Mkutano Mkuu wa jumuiya ya Watanzania Rome ambao uliokuwa unasubiliwa na wengi, jana jioni (19 Nov.)ulifanyika kwenye ukumbi uliopo Via cassalattico 6, maeneo ya Grottarossa-assia.
Mkutano ulianza na wimbo wa Taifa kama desturi ya jumuiya. Baada ya wimbo wa Taifa, wanajumuiya na wageni waalikwa walijitambulisha. Hili ni muhimu haswa kwa sisi tulio nje ya nchi, maana linatuwezesha kufahamiana kwa ukaribu zaidi.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Rome, Mheshimiwa Leonce Uwandameno alifungua mkutano kwa kueleza muhtasari na kisha kumkaribisha katibu wa jumuiya ndugu Andrew Chole Mhella kuelezea mafanikio mbalimbali yaliyotokea kwenye kipindi cha mwaka mzima. Mafanikio ambayo ndugu katibu alielezea ni yafuatayo:
Kwanza kabisa, kwenye kipindi cha mwaka uliopita, Jumuiya ya Watanzania Rome imefanikiwa kuitangaza Tanzania kwa wenyeji wetu hapa Italia. Mafanikio ya kuitangaza Tanzania yalitokana na mikakati kadhaa kama vile jumuiya ilipoandaa SIKU YA UTAMADUNI WA TANZANIA.
Pili, Jumuiya pia ilifanikiwa kushirikiana na jumuiya mbalimbali za Watanzania hapa Italy na zaidi NGOs za kitaliano zinazo fanya kazi nchini Tanzania kwenye maswala mbalimbali.
Tatu, Jumuiya pia inafuraha kuwajulisha pia kwenye mwaka ulioisha imefanikiwa pia kufungua Account ambapo kwa wale ambao hawataweza kufikisha michango yao kwa mweka hazina wanaweza kudeposit michago moja kwa moja kwenye account ya Jumuiya.

katika mkutano wa jana pia kulikuwa kuwe na uchaguzi mkuu wa viongozi wapya kwa mujibu wa katiba. Lakini kutokana na wanajumuiya hai kutofikia idadi inayotakiwa kikatiba, uchaguzi uliahirishwa mpaka hapo itakapotamgazwa tena.

Andrew Chole Mhella,
Katibu wa Jumuiya ya Watanzania Rome.



No comments:

Post a Comment