Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Wednesday, October 13, 2010

Kumbukumbu ya Baba wa Taifa (13 April 1922- 14 October 1999)






















JUMUIYA YA WATANZANIA ROMA, inaungana na Watanzania dunia kote kwenye kuadhimisha kumbukumbu za mwaka wa kumi na moja za kifo cha Baba wa Taifa Letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Baba wa Taifa ambaye mafunzo yake yamebakia mioyoni mwa kila mtanzania na wapenda amani duniani, alifariki dunia tarehe 14 Oktoba 1999 kwenye ospitali ya Mtakatifu Thomas nchini Uingereza, ambako alikuwa akitibiwa. Kifo cha Baba wa Taifa kimetuachia pengo ambalo alitazibika, ila kitu muhimu kwa sisi Watanzania ni kumuenzi kwa kuyafuata yale ambayo alikuwa anatufundisha. Baba wa Taifa alitufundisha mengi, ambapo mengi yake ndio yamebaki kama msingi wa taifa letu. Itakumbukwa kuwa, Baba wa Taifa alitufundisha umuhimu wa kupendana kama watanzania na kuondoa kabisa ukabila udini na uadui wa aina yeyote ile maana ndivyo huwa ni vyanzo vya mvurugani nchini.
JUMUIYA YA WATANZANIA ROMA, inapenda kuwasihi watanzania kufuata wosia ambao baba wa Taifa alituachia zaidi kwenye mwezi huu wa uchaguzi, ili uchaguzi uwe wa amani na utulivu kama alivyokuwa anapenda Baba wa Taifa.

Watanzania tuishio hapa Rome, na wengine waliotoka sehemu mbalimbali za Italy, miaka ya nyuma (1995) tulibahatika kupata ugeni wa Baba wa Taifa, ambaye alikuja Italy kwaajiri ya kutunukiwa shahada la heshima na kwa upendo wake alitupa fursa ya kukutana nae na kupata chakula cha mchana kwa pamoja kwenye collegio S. Peters licha ya kuwa na ratiba ngumu.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Africa.

No comments:

Post a Comment