Pages

log with Fire

WELCOME TO TANZANIA
Tanzanian Community in Rome, Via GIUSEPPE DI VITTORIO 9, 00067 MORLUPO, Rome, Italy -- Sasa Mnaweza kuweka Michango yenu ya mwezi kwenye account ya Jumuiya: Banki ya Posta:Associazione dei Tanzaniani a Roma Acc. Number 000007564174 Codice Fiscale: 97600810580 ---

welcome to Tanzania

TANZANIAN COMMUNITY IN ROME (TZ-RM,) is a community that unites TANZANIANS living in Rome and those living outside of Rome who have read, understood and accepted the content of its Constitution and hence becoming part of the community's family. Tanzanian Community in Rome is a fruit of the well designed ideas, approved by all community members at the Community's First General Meeting held on the 30th January, 2010. It is a non-political, non-religious, non-ethnical and non-gender based kind of organization. It is a community that democratically, accepts and respects different ideas from all its members without any sort of segregation.

Tanzanian Community in Rome counts alot on members monthly contributions in order to keep the community alive.But all in all, it appreciates any sort of contribution from anyone.

Wednesday, June 23, 2010

JUMUIYA YA WATANZANIA ROMA YAJITAMBULISHA RASMI KWENYE UBALOZI WA TANZANIA NCHINI ITALY


Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania mjini Rome, Mh. Leonce Uwandameno, katikati afisa wa Utawala Ubalozi wa Tanzania nchini Italy, Mh. Salvator Mbilinyi, na kulia ni Katibu wa Jumuiya ya Watanzania Rome, Ndugu Andrew Chole Mhella

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Roma Mh. Leonce Uwandameno pamoja na Katibu wake Ndg. Andrew Chole Mhella, leo asubuhi, tarehe 23 Juni 2010, waliwasilisha rasmi barua ya utambulisho wa Jumuiya ya Watanzania Roma kwenye ubalozi wa Tanzania nchini Italy. Viongozi hawa walipokelewa na afisa utawala wa ubalozi Mh. Salvator Mbilinyi. Itakumbukwa kuwa jumuiya hii ya Watanzania Roma, iliundwa rasmi mjini Rome tarehe 30 Januari 2010. Moja ya malengo mengi ya uundwaji wa Jumuiya hii ni; kuwaunganisha watanzania wanaoishi Roma na sehemu zingine za Italy, ili kushikamana na kusaidiana panapo kuwa na furaha au tatizo la aina yoyote. Jumuiya inalenga kuhamasisha wanajumuiya ili waweze kuishi kwa malengo hapa ugenini na kupeleka maendeleo nchini Tanzania. Jumuiya hii pia inalengo la kuwa chombo cha kuutangaza utamaduni na utalii wa nchi yetu hapa nchini Italia.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Jumuiya ya Watanzania Roma.

Kwa matukio mbalimbali yanayotokea hapa Rome, mnakaribishwa kwenye official blog ya Jumuiya www.watanzania-roma.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment