Mwili wa mpendwa wetu,ndugu yetu Moses Kiumbi(Ama Mzee kama alivyofahamika sana huku nyumbani) uliwasili Tanzania Jumanne usiku.Sala ya marehemu ilifanyika nyumbani kwao Mwenge Dar es salaam kabla ya kuelekea Mkuranga mkoa wa Pwani(Shambani kwa baba yake)kwa mazishi.Mbali na ndugu jamaa na marafiki washio Tanzania tulipata bahati ya kujumuika na ndugu Abdulrahaman Alli katika mazishi hayo. Mh Abdulrahaman Alli ni Mwenyekiti wa jumuiya ya Watanzania Italy
Napenda kuchukua nafasi hii kuushukuru uongozi mzima wa jumuiya ya Watanzania Italy na Watanzania wote waishio Italy kwa ushirikiano wenu mpaka kuufikisha mwili wa marehemu ndugu yetu nyumbani kwa mazishi, hatuna cha kuwalipa Mungu ndie ajuae malipo yenu. Nawatakia kila la heri.
Wenu,
Hassan B. Yusuf (Moses's causin brother) TANZANIA.
Source: www.tnzncommunity.blogspot.com
No comments:
Post a Comment